March 14, 2013




 
Upasuaji wa uvimbe wa shavu wa beki wa Yanga, Ladislaus Mbogo umekwenda vizuri na afya yake inaendelea vizuri katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Salehjembe imemshudia Mbogo akiwa katika hospitali hiyo, na leo asubuhi wachezaji wa Yanga, mara baada ya mazoezi ya asubuhi walikwenda kumtembelea.

Upasuaji wa uvimbe wa Mbogo aliyejiunga na Yanga akitokea Toto African ulifanyika chini wa daktari wa timu hiyo, Nassor Matuzya.

Mbogo amesema anajisikia vizuri baada ya kushituka, jana alizinduka kutoka usingizini saa 11 jioni, baada ya kufanyiwa upasuaji huo kwa zaidi ya saa tatu.

Wachezaji wa Yanga walimtembelea na kuzungumza naye huku wakitaniana, lakini walilazimika kuingia kwa makundi kutokana na wingi wao.

Gazeti la Championi lilikuwa la kwanza kuandika kuwa Mbogo atafanyiwa upasuaji.
Blog hii pia ilikuwa ya kwanza kutaarifu kuhusiana na hilo na Mbogo maarufu kama Mnyama sasa atakuwa katika muonekano tofauti.

Hata hivyo, daktari mmoja katika hospitali ya Mwananyamala, alisema muonekano wake utabadilika taratibu kulingana na ngozi inavyosinyaa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic