April 9, 2013




Morad, Nyoni na Aggrey wakiwa na kipa Mwadini

Uongozi wa klabu ya Azam FC, leo umetangaza kuwarudisha wachezaji wake waliokuwa wanatuhumiwa kuchukua rushwa.

Azam FC imeeleza kwamba imepata taarifa kutoka Takukuru kuwa wachezaji  hao wameonekana hawana hatia.


Katika ripoti hiyo iliyotolewa na katibu Mkuu wa Azam FC, Nassor Idrissa, Azam imeeleza kuwarudisha kundini.
  Azam FC inatoa taarifa rasmi kuwa Takukuru haijawakuta na hatia ya rushwa wachezaji Deogratius Munish, Erasto Nyoni, Said Hussein Morad na Agrey Morris,” ilieleza sehemu ya ripoti hiyo.

“Hivyo wachezaji hao wanakaribishwa rasmi kurudi kikosini Azam FC kwa ajili ya kujiunga na mazoezi na wachezaji wenzao.”
Azam iliwatuhumu wachezaji hao kupokea rushwa katika mechi dhidi ya Simba, hivyo ikaamua kulifikisha tukio hilo Takukuru.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic