Simon Msuva na Frank Domayo wa Yanga na Taifa Stars baada ya mazoezi ya Yanga.. |
*Wako wanaopanda
mishikaki kwenye bodaboda
Na Saleh
Ally
TAKRIBANI
wiki nne nilikuwa kwenye mazoezi ya asubuhi, ilikuwa kwenye Viwanja vya Leders,
nikashuhudia kitu ambacho kilinishangaza kiasi fulani.
Siku chache
baadaye, nilikuwa katika mazoezi ya Yanga kwenye Uwanja wa Bora Kijitonyama
jijni Dar, nikaona kitu kama nilichokiona katika mazoezi ya Simba, nitakueleza.
Kila baada
ya mazoezi ya timu hizo mbili kubwa kumalizika kunakuwa na usafiri wa basi
ambao unatolewa na uongozi kwa ajili ya wachezaji hao. Lakini kawaida wengi
hawapendi kupanda pamoja katika basi hilo.
Rashid Mkoko wa Simba baada ya mazoezi.. |
Wengi
wanachumua usafiri binafsi, ukianza na wale wenye usafiri wao binafsi na baada
ya hapo wale wanaokodi Taxi, Bajaj au Bodaboda kurejea makwao. Si kitu kibaya,
lakini kuna maswali kadhaa nikaanza kujiuliza.
Maswali
yangu yalianza baada ya kuona wachezaji wa Simba wanapanda Bajaj na wale wa
Yanga pia, ingawa Simon Msuva na Frank Domayo ndiyo walinishitua zaidi baada ya
kupanda pikipiki moja maarufu kama ‘mshikaki’. Siku chache nilimuona Rashid
Ismail Mkoko akipanda Bajaj.
Yaani
Domayo na Msuva wa Yanga, wamepanda mshikaki! Acha tu kwamba ni wachezaji wa
Yanga, lakini ni wachezaji wa kikosi cha timu ya taifa , Taifa Stars!
Sitaki
nionekane ninadharau usafiri wa Bodaboda na Bajaj, lakini najaribu kuonyesha
kiasi gani uongozi wa klabu hizo mbili unavyoweza kufanya na kubadilisha mambo.
Hakuna ubishi kupanda mshikaki katika Bajaji ni kuvunja sheria, lakini ni
hatari sana kwa afya ya wahusika.
Msuva na
Domayo leo ni tegemeo la Wanayanga ambao wako zaidi ya milioni 10 nchini,
lakini pia ni tegemeo kwa taifa letu lenye watu zaidi ya milioni 40. Sasa vipi
wapande kwenye pikipiki, tena mshikaki!
Sitaki
kuwafananisha wachezaji hao wa Yanga na Simba sawa na wale wa Man United kama
Wayne Rooney, Cristiano Ronaldo (Real Madrid) na wengine. Lakini kuna sehemu
inafikia, mchezaji anatakiwa kuwa na usafiri wake binafsi.
Pele
aliwahi kusema, gari lake aina ya Mercedes Benz ambalo alihofia kulinunua,
liligeuka na kuwa changamoto ya kumshawishi acheze vizuri kwa kuwa alihofia
akiharibu, basi atalazimika kuliuza, ila akijituma, atapata fedha za kununua
gari bora zaidi ya alilokuwa nalo.
Ninaamini
inawezekana kabisa mambo yakaenda tena vizuri bila ya wachezaji hao kupanda
mshikaji kwenye pikipiki na ubunifu ukifanyika unaweza kubadili hali hiyo.
Klabu:
Klabu
nyingi za Ulaya zimeingia mkataba wa kuyatangaza makampuni ya magari ambayo
pamoja na mamilioni ya fedha zinazotoa kama watangazaji, lakini zinatoa magari
kwa wachezaji wa timu hizo kwa bei nzuri yenye unafuu mkubwa.
Mfano mzuri
ni Real Madrid na Man United zinazotangaza magari ya Audi, Arsenal na Citroen
na Liverpool na Chevrolet.
Hapa
inawezekana, hata kama kwa makampuni yanayouza magari yaliyotumika
yakajitangaza na Yanga au Simba na mwisho nayo yakatoa punguzo kubwa kwa wachezaji
watakaotaka magari. Hapa siku ya mwisho, klabu, watangazaji na wachezaji, wote
wanafaidika.
Wachezaji:
Hadi
kufikia kucheza katika klabu kubwa au timu ya taifa, gari haiwezi kuwa starehe
tena. Ni wajibu kwa kuwa kuna mambo kadhaa mchezaji anatakiwa kuyafanya.
Mfano,
baada ya mazoezi, anatakiwa kuingia kwenye gari lake na kwenda nyumbani
kupumzika. Lakini si kugombea daladala, au kuhangaika kuuma meno akiwa
amemkumbatia dereva wa bodaboda.
Mara nyingi
wanafanya mazoezi mara mbili kwa siku, jiulize safari ya kwenda na baadaye
kurudi tena mazoezini kwa kugombea usafiri wa jamii. Nafikiri inabidi mlifanyie
kazi hilo na inawezekana tu.
Gari si
ufahari tena, inawezekana mkanunua za bei nafuu kwa ajili ya kusaidia utendaji
wenu lakini kuendana na mlipofikia.
SOURCE:
CHAMPIONI NEWSPAPER
ushauri mzuri sana
ReplyDelete