May 14, 2013




Kipigo cha mabao 4-1 walichokitoa Arsenal kwa Wigan Athletic maana yake timu hiyo ‘roho ya paka’ imeteremka daraja.

Wigan ambao ni mabingwa wa Kombe la FA wameteremka daraja baada ya kipigo hicho katika Uwanja wa Emirates jijini London.


Wigan ilikuwa inataka ushindi ili ibaki na Arsenal ilitaka ushindi ili ipate nafasi ya nne na ikiwezekana kuendelea kugombea nafasi ya tatu katika mechi moja ya mwisho iliyobaki.



Wigan imekuwa ikipambana karibu kila msimu kuwania kutoteremka daraja, lakini leo ilikuwa siku mbaya kwao.

Wigan imeungana na Reading na QPR kukamilisha timu tatu zilizoteremka daraja msimu huu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic