May 15, 2013



Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi amesitisha uamuzi wa kuendelea na matibabu, televisheni ya Catalan ya Channel 'TV3' imeeleza.
Alitakiwa kwenda hospitali juzi asubuhi lakini hakufanya hivyo na alitakiwa kuchukuliwa kipimo cha MRI kwa ajili ya kuendelea na matibabu.

Hospitali hiyo ya Creu Blanca ndiyo ilikuwa ikimpatia matibabu na imekuwa ikishughulika na matibabu ya wanamichezo mbalimbali.
Uamuzi wake wa kugoma kuendelea na matibabu katika hospitali hiyo umewashangaza watu wengi lakini Messi akashikilia msimamo wake.

Kutokana na hali hiyo, madaktari wa Barcelona walilazimika kuwasiliana na uongozi ambao ulifanya mawasiliano na Messi ambaye alishikilia msimamo huo.


Baadaye walipojadiliana, walikubalia Messi afanyiwe vipimo katika kituo maalum cha mambo ya afya kinachomilikiwa na Barcelona.
Ingawa uongozi wa Catalunya haujathibitisha kuhusiana na nilo lakini kweli Messi alifanyiwa vipimo Sant Joan DespĂ­ inayomilikiwa na klabu hiyo.

Hivi karibuni Messi amekuwa akisumbuliwa na maumivu hali inayosababisha asiwe katika hali yake ya kawaida.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic