May 16, 2013



Chelsea imefanikiwa kutwaa Kombe la Europa League baada ya kuichapa Benfica ya Ureno kwa mabao 2-1.

Katika mechi hiyo ya fainali iliyopigwa mjini Amsterdam nchini Uholanzi, Chelsea walipata mabao yao kupitia kwa Fernando Torres na Branislav Inavovic na Benfica wakapata hilo moja kupitia Cardozo.




Torres aliichambua ngome ya Benfica hadi kipa kabla ya kupachika bao na Cardozo akafunga kwa mkwaju wa penalty baada ya Azpilicueta kunawa mpira ndani ya 18.





Lakini ikionekana kama mechi ndiyo imemalizika, Ivanovic alifunga kwa kichwa baada ya kona kuchongwa wakati mwamuzi wa akipa akiwa ameinua ubao kuonyesha dakika 90 zimekamilika.





Baada ya bao hilo, machozi ya mashabiki na wachezaji wa Benfica yalitawala uwanjani hapo, kwani karibu kila mmoja alishindwa kujizuia na kububujikwa na machozi.

Kocha Rafa Benitez ambaye alikuwa hatakiwi na mashabiki wa Chelsea naye alikuwa na furaha kubwa baada ya ushindi huo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic