May 15, 2013




Pamoja na kubariwa na maumivu mwili mzima, beki kisiki wa Real Madrid, Sergio Ramos huenda akacheza katika mechi ya fainali ya Copa del Rey dhidi ya Atletico Madri, kesho Ijumaa.

Ingawa Madrid wamefanya jambo hilo siri kubwa, lakini kuna taarifa watalazimika kumtumia Ramos kutokana na ushawishi wake uwanjani.

Kumekuwa kuna juhudi za makusudi ili kuhakikisha mwili wa Ramos unarudi katika hali nzuri ingawa inaonekana hatakuwa fiti kwa asilimia mia.

Ramos amekosa mechi nyingine za Madrid ilipokutana na Valladolid, Málaga na Espanyol. Lakini amekuwa chini ya uangalizi ili acheze mechi hiyo.

Kitu kingine kinachofanya Madrid ilazimike kuhakikisha Ramos anacheza ni kukosekana kwa Raphael Varane raia wa Ufaransa aliyefanyiwa upasuaji.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic