May 8, 2013



 
Mlezi wa Simba, Rahma Al Kharusi amefanya kazi ya ziada kumshawishi mmiliki wa Sunderland kukubali kuisaidia klabu hiyo.


Katika mazungumzo kati ya Ellis Short, bilionea mmiliki wa Sunderland na Rahma maarufu kama Malkia wa nyuki, mafanikio yamekuwa makubwa sana.

Ingawa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage aliongozana na mwanamama huyo, lakini ushawishi mkubwa ulitoka kwake.


Kwani ndiye aliyetoa maombi ya wachezaji kupata nafasi ya kufanya majaribio Sunderland, makocha wao kujifunza na pia kuanzishwa kwa Academy.

Short amekubali mambo yote kimsingi, maana yake ni suala la Simba kuitumia vizuri nafasi hiyo waliyoipata kwa ushawishi wa mwanamama huyo mwanamichezo.

Simba imeruhusiwa kupeleka wachezaji kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu England.
Ukichana na hivyo, itapata fursa ya kujengewa uwanja wa mazoezi ambao zaidi utatumiwa na timu za watoto kuanzia miaka mitano hadi 11 na baadaye hadi chini ya miaka 16.


Kupitia Sunderland na maombi yaliyotolewa na Malkia wa nyuki maana yake, Simba ndiyo watafaidika zaidi kwa kuwa na urafiki na klabu hiyo.
Huenda kutotanguliza fedha kwanza kama msaada namba moja kumeisaidia Simba kupata mambo yote hayo.


Kwani kama yatatumika vizuri, maana yake yanaweza kuisaidia klabu hiyo kupata fedha nyingi zaidi hapo baadaye.

Huenda kikaonekana ni kama kitu kidogo tu, lakini alichokifanya Malkia wa nyuki si kitu kidogo na kinatakiwa kulindwa vilivyo.

Kukilinda kwake ni watu kufanya utekelezaji bila ya kuvunja makubaliano na wazungu hao, kwani kama watakiuika, basi ndiyo utakuwa mwisho wa makubaliano na hasara itabaki kuwa kwa Simba.

Lakini kama wataitumia nafasi hiyo vizuri, itakuwa ni faida kubwa lakini wataonyesha wameelewa alichokitaka Malkia wa nyuki ambaye ameangalia mbele zaidi badala ya fedha kwa ajili ya leo pekee bila ya kujua kesho ukiamka utajiendesha kwa kutumia fungu lipi.


Huenda Malkia angebaki kwake na kuendelea na biashara zake, au kujumuika na familia yake lakini amekubali kusafiri maelfu ya kilomita kwenda kuipigania Simba huko England.

Hakika ni kitu cha kumpongeza, lakini itakuwa faraja kwake kama makubaliano hayo yatatumiwa vizuri na uongozi wa Simba.


Iwapo longolongo itaingia katikati, kwanza kabisa itakuwa ni kumkatisha tamaa kwa kiasi kikubwa na huenda ataanza kukumbuka hasi, kwamba alipoteza muda wake.

Pili, mtamuabisha, maana alichokiomba hakitafanyika na mwisho itaonekana yuko kwenye kundi lenu la kubahatisha.

Makubaliano ya uhusiano na Sunderland si kitu kidogo kwa kuwa imepiga hatua tena mbali kwa maendeleo ya soka na Simba imepata bahati ya mtende. Vema ikaitumia kwa manufaa ya klabu na si wajanja wachache wanaojua kuzungusha maneno mdomoni, huku mikono yao inachota mali za klabu.

3 COMMENTS:

  1. Simba hiko vizuri sana , sasa hapo fitina na majungu ziwekwe pembeni watu wafanye maendeleo

    ReplyDelete
  2. She is a lady of deeds than words she deserves our thanks for her vision and to care for the development of others.

    ReplyDelete
  3. Nimeipenda hii. Well done Malkia wa Nyuki!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic