Baada ya kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Simba leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, uongozi wa Mgambo ya Tanga umelia kuonewa.
Katibu Mkuu wa Mgambo, Anthony Mgaya amesema waamuzi hasa wale wasaidizi waliokuwa na vibendera waliwaonea.
Mgaya amesema mwamuzi aliyekuwa na kibendera alionyesha kupania wao wapoteze mchezo.
“Bao tumefungwa halali kabisa, lakini kweli mwamuzi alikuwa ni tatizo kubwa kwetu.
“Lakini ndiyo hivyo tunakubali matokeo lakini hilo halijatufurahisha kwa kweli,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment