May 15, 2013


Milovan akiwa na Barthez wakati akiwa Simba....

Na Saleh Ally
KOCHA wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic, ameamua kufungua mdomo wake kwa mara ya kwanza na kuizungumzia mechi ya watani, Yanga na Simba inayotarajiwa kuchezwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Milovan, raia wa Serbia, amesema huenda Yanga wakawa wanajidanganya kwa kuamini Simba ni rahisi kwa kuwa inatumia wachezaji vijana, kitu ambacho si sahihi.


Akizungumza kutoka Cacak, Serbia, Milovan alisema mechi hiyo itakuwa ngumu na si kama namna watu wanavyoichukulia kirahisi.

“Bado Simba wana timu nzuri ya kushindana, wanaweza kupambana na kufanya vizuri, sidhani kama itakuwa kama wanavyoamini mashabiki.

“Vijana walio Simba uwezo wao ni mzuri na wanaweza kupambana na kufanya vizuri. Si sahihi kuwachukulia kwamba watapoteza.

“Lakini pia Simba ili wafanye vizuri, hawapaswi kuwa waoga, badala yake wanatakiwa kupambana kama wanaume. Soka ni mchezo wa wanaume,” alisema Milovan.

Milovan ndiye kocha aliyeiongoza Simba kuweka rekodi nyingine kwa kuichapa Yanga kwa mabao 5-0 katika mechi ya mwisho ya kufunga msimu uliopita huku ikiwa tayari imeshabeba ubingwa.

Katika mechi ya watani hao mzunguko wa kwanza, matokeo yalikuwa sare ya bao 1-1, Yanga wakisawazisha kupitia Said Bahanuzi kwa mkwaju wa penalti baada ya bao la mapema la Amri Kiemba.

Mechi hiyo ya bao 1-1 ilikuwa ya Milovan ambaye alifutwa kazi na nafasi yake kuchukuliwa na Mfaransa, Patrick Liewig, atakayekuwa anapambana katika benchi Jumamosi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic