Kocha mpya wa Manchester United, David Moyes mwenye
umri wa miaka 50, atajiunga rasmi na klabu yake hiyo mpya Julai Mosi na kuanza
kazi.
Moyes aliyesaini mkataba wa miaka sita kuifundisha
Manchester United baada ya kujiuzulu kwa Alex Ferguson, mechi yake ya kwanza ya
mashinda itakuwa kati ya wapinzani wakubwa wa Man United, Manchester City au
Wigan.
Mechi hiyo itachezwa Agosti 11 kwenye Uwanja Wembley
jijini wakati wa mchezo wa ngao ya jamii.
Akizungumza kwa mara ya kwanza baada ya kuingia
mkataba huo wa miaka sita kuchukua nafasi hiyo ‘nzito’ ya Ferguson, Moyes
alisema: “Ni heshima kubwa kuchaguliwa kushika nafasi ya Ferguson, ninaamini
atakuwa amnipendekeza kuwa hapa.
“Nina heshima kubwa na alichofanya katika soka kama
kocha. Nasikia raha kuchukua nafasi baada ya kocha bora kabisa duniani, lakini
pia bahati ya kuinoa klabu kubwa kama Manchester United. Nina matumaini makubwa
ya kufanya vizuri.”
“Nawashukuru sana Everton ambao nimefanya nao kazi
kwa muda mrefu sana na wamekuwa watu wazuri na waliochangia mafanikio yangu
hadi kufikia hapa nilipo, nawashukuru sana.”
Mechi dhidi ya Manchester City kama wakiwa mabingwa
wa FA itakuwa ni mtihani mgumu kwa Moyes ambaye atakuwa ametoka katika mechi za
maandalizi kujiandaa na msimu mpya na tayari atakuwa ameingoza timu hiyo katika
mechi za kujipima nguvu na kuandaa kikosi.
nadhani bado haijajulikana kama itakuwa man u au wigan hapa utakuwa umewajudge vibaya wigan bro
ReplyDelete