May 8, 2013


Msuva (kushoto) na Luhende...


Na Saleh Ally
Yanga imeingia katika karne nyingine ya maamuzi baada ya kuwachata mshahara wachezaji wake wawili, Simon Msuva na David Luhende.
Msuva na Luhende, kila mmoja amekatwa Sh 200,000 kutokana na kupatikana na hatia ya kucheza mechi za mchangani maarufu kama ndondo.

Habari za uhakika kutoka ndani ya klabu ya Yanga zinaeleza, Msuva na Luhende ‘walijiachia’ na kuchezea timu za mtaani kwao katika michuano ya mchangani kitu ambacho kimekatazwa na uongozi wa Yanga.


“Ukiachana na uongozi kukataza, lakini suala hilo liko katika mikataba yao. Unaweza kusema wamekiunga mikataba, ndiyo maana utaona adhabu imekuwa kubwa ili iwe mfano kwa wengine.

“Luhende alikuwa akimlalamikia kocha kwamba fedha alizokatwa ni nyingi sana, lakini uongozi na hata kocha mwenyewe tumesisitiza adhabu iendelee kubaki hivi,” kilieleza chanzo.

Ingawa wachezaji hao hawakutaka kulizungumzia suala hilo, lakini Yanga imeahidi kupambana na tatizo hilo la wachezaji wake kucheza mechi za mchangani.

Uamuzi huo unatokana na baadhi ya wachezaji kugundulika huumia wakiwa katika mechi zao hizo za ndondo lakini klabu inaingia gharama kuwatimu.

Tatizo la wachezaji kucheza mechi za mchangani kwa ajili ya kujipatia malipo ya ziada limeendelea kuwa kubwa katika timu mbalimbali za ligi kuu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic