May 15, 2013



 
Tchetche akishangilia na Agrey Morris..
Kocha Mkuu wa Azam FC, Stewart Hall ametia ruhusa kwa wachezaji wote wageni kurudi makwao.

Wachezaji wa kigeni wanaokipiga Azam FC ni Kipre Tchetche aliyeibuka mfungaji bora, ndugu yake Bolou Tchetche, wote raia wa Ivory Coast.
Wengine ni Humprey Mieno, Jockins Atudo (wote Kenya) na  Bryan Umonyi kutoka Uganda. 


Hall raia wa Uingereza ameamua kuwatumia wachezaji wazalendo tu katika mechi ya mwisho ya Ligi Kuu Bara ambayo watacheza dhidi ya JKT Oljoro wakiwa ugenini jijini Arusha, Jumamosi.

Uamuzi wa Hall umelenga kuwapa nafasi wachezaji wazalendo hasa wale ambao hawakupata nafasi.

“Tunaweza kuwatumia wazalendo katika mechi hiyo, tunajua tukishinda au kupoteza tutabaki katika nafasi ya pili.

“Lakini bado tunauchukulia mchezo huo kwa ukubwa kwa kuwa pointi zitatufanya tusiwe na pengo kubwa dhidi ya Yanga.

“Tunawaamini wachezaji wazalendo na nimewapa nafasi hivyo ni vizuri wakaitumia,” alisema.

Msemaji wa Azam FC, Jaffar Idd Maganga alisema baadhi ya wachezaji wageni walishaanza kuondoka nchini mara moja baada ya kupata ruhusa hiyo ya Hall.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic