Simba wameanza juhudi ya kulikomboa basi
lao linaloshikiliwa na kampuni ya MEM Auction.
Simba ilikuwa inadaiwa Sh milioni 42
lakini ikalipa Sh milioni 22, hivyo bado inadaiwa Sh milioni nane.
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage
amethibitisha kukamtwa kwa basi lao na amesema wameanza juhudi za kulikomboa.
“Kweli limekamatwa na tunaendelea
kulifanyia kazi ili kulikomboa,” alisema.
Basi hilo Simba walipewa na wadhamini
wao Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia udhamini wake wa Bia ya Kilimanjaro.
0 COMMENTS:
Post a Comment