Mwenyekiti wa Simba, aliyesimamishwa,
Ismail Aden Rage amewarudisha kazini makocha Abdallah Kibadeni na Jamhuri
Kiwhelo ‘Julio’.
Rage ametangaza leo kwamba Kibadeni na Julio
wataendelea na kazi yao na si kocha Logarusic.
Baada ya rage kusimamishwa na kamati ya
utendaji ilitangaza kuwaondoa makocha hao na nafasi yao kuchukuliwa na
Logarusic raia wa Croatia lakini Rage na akawapinga na kujirudisha madarakani.
Mgogoro ndani ya Simba unazidi kuwa
mkubwa kwani Rage amekuwa na upande wake huku kamati ya utendaji nayo
ikisimamia upande wake.
“Kweli nimewarudisha Kibadeni na Julio
na hawa ndiyo makocha wa Simba na wataendelea na kazi,” alisema Rage leo hii.
0 COMMENTS:
Post a Comment