Mshambuliaji wa Simba, Betram Mwombeki,
ameonyesha kuwazidi nyota wenzake wa kikosi hicho kwa kuendelea kujifua katika
mazoezi yake binafsi ambayo yamemghalimu kulipa kiasi fulani cha fedha.
Mwombeki amesema katika mazoezi yake hayo anayoyafanya jijini Mwanza, amekuwa
akimlipa Sh 50,000 kwa wiki kocha maalum anayemnoa, Athuman Bilal.
Mwombeki amesema tayari ameshajifua kwa
wiki tatu sasa ambapo mazoezi hayo yataendelea mpaka kukaribia kwa ufunguzi wa
kambi ya kikosi hicho, ambacho kinatarajiwa kuanza rasmi maandalizi Desemba
Mosi kikiwa na kocha mpya, Mcroatia, Zdravok Logarusic.
“Nimepanga kujiweka sawa, unajua huku
nipo na kocha wangu Bilal (Athuman) na nimekuwa nikimlipa shilingi elfu hamsini
kwa wiki, nataka kuwa tayari kabla ya kuja kwenye mazoezi ya timu nzima,”
alisema Mwombeki.
“Mpaka sasa nimeshakuwa kwenye mazoezi haya
kwa wiki tatu sasa, nitaendelea hivi mpaka kukaribia kwa kambi ya timu nzima,
wakati naanza nilikuwa nafanya kwa siku mara mbili lakini wiki hii (iliyopita)
nimeanza kufanya mara moja kwa siku.”
Mwombeki ameumaliza mzunguko wa kwanza
wa Ligi Kuu Bara akiwa amefunga mabao manne.
SOURCE: CHAMPIONI
0 COMMENTS:
Post a Comment