Nahodha wa pembeni na nahodha wa Simba,
Said Nassor ‘Chollo’, amewashauri viongozi wa klabu hiyo wahakikishe wanamnasa
kipa Ivo Mapunda anayeichezea Gor Mahia ya Kenya.
Simba inadaiwa kumhitaji kipa huyo katika
usajili huu unaoendelea kwenye Ligi Kuu Bara.
Ivo anatarajiwa kumaliza mkataba wake na
Gor Mahia mwezi ujao na Simba inahitaji kipa kutokana na Abel Dhaira kushindwa
kukata kiu ya mashabiki katika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara.
Chollo alisema kutokana na kiwango alichonacho Ivo ukichanganya na uzoefu
alionao kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, litakuwa ni jambo jema kama akitua
Msimbazi.
“Bado ni golikipa mzuri kwa uwezo wake
niliouona kwenye mechi ya Taifa Stars dhidi ya Zimbabwe, halafu ukizingatia
ameipa ubingwa Gor Mahia, kwa hiyo ni mtu anayefaa, itakuwa ni vizuri kama
akija tusaidiane kuipeleka Simba mbali zaidi,” alisema Chollo.
0 COMMENTS:
Post a Comment