Kipa namba moja wa Yanga, Deogratius
Munishi ‘Dida’, ameeleza kuwa katika mchezo wa leo dhidi ya Simba, atahakikisha
mshambuliaji Amissi Tambwe hapati bao.
Dida anatarajiwa kukaa langoni leo
katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu Bara msimu huu dhidi ya watani wao wa jadi
Simba kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Dida
amesema atawapanga vizuri mabeki wake kuhakikisha Tambwe hafungi bao lolote
hata la kuotea.
“Ninajua mchezo utakuwa mgumu lakini
nina imani mabeki wangu watanilinda vizuri na kuhakikisha wanazuia kikamilifu
mashambulizi ya Simba na kutotoa nafasi kwa Tambwe kufunga bao lolote.
0 COMMENTS:
Post a Comment