MOJA YA MAGARI BAADA YA SHAMBULIZI LA JANA. |
Pamoja na kikosi chake kufanikiwa kuingia hatua ya 16 Bora ya Kombe la
Dunia, Kocha wa Nigeria, Steven Keshi ameonekana kutokuwa na furaha.
Shambulizi la mwisho ni jana wakati Nigeria ilipofungwa mabao 3-2 na
Argentina, lakini ikasonga mbele.
KESHI |
Watu 16 wameuwawa katika shambulizi hilo la bomu jijini Abuja.
“Sielewi wanafanya nini hawa watu, hawajui wanauwa watu wasiokuwa na
hatia,” alihoji Keshi.
Kabla ya mechi hiyo, wakati Nigeria ikicheza mechi dhidi ya Iran, pia
walifanya shambulizi na kuuwa watu 14.
Mashabiki wa Nigeria wamekuwa wakilaani mashambulizi hayo ya Boko Haram waliojichimbia Kaskazini mwa nchi hiyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment