Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeitaka klabu ya
Yanga kuwasilisha rasimu ya Katiba waliyoipitisha, kwa kuzingatia kuwa
Muhtasari wa kikao cha Mkutano Mkuu wao wa Juni 1 mwaka huu umeainisha baadhi
ya marekebisho waliyofanya kwa tulivyowaelekeza.
Yanga chini ya Yusuf Manji wanatakiwa kuwasilisha rasimu hiyo kabla ya Oktoba 5 mwaka
huu.
Ikiwa itakubaliwa na TFF, itapelekwa kwa Msajili wa Klabu na Vyama vya
Michezo ili waweze kufanya uchaguzi wa viongozi wao.
0 COMMENTS:
Post a Comment