October 4, 2014


FULL TIME: Dk 90+4
Dk 90, Simba inapata kona tatu mfululizo, lakini hakuna lolote.

Dk83, Maguli tena anashindwa kufunga baada ya kupiga kichwa, mpira unapaa puuu.


Dk 77 Saidi Mohamed anapigwa shuti, linaokolewa na kuwa kona.

Dk 72, Maguli anapiga shuti kali lakini linadakwa kiufundi.
Dk 65, Okwi anapiga mpira unagonga mwamba na kutoka nje.


Dk 62, Mobi anapiga shuti lakini linatoka juu kidogo juu ya lango la Simba.


Dk 61, Ndemla anapiga shuti kali lakini linaguswa na kupaa nje( anagusa mchezaji mwenzake)


Dk 59, Okwi tena anashindwa kufunga baada ya mpira mzuri wa kona kumkuta akiwa pekee...Stand wanaonekana kujilinda zaidi.


Dk 58, Tambwe anapiga kichwa safi kabisa lakini kipa wa Stand anaugusa na unagonga mwamba na kurudi uwanjani.

Dk 56, Simba ndiyo wanashambulia zaidi, nafasi nyingine anapoteza Okwi.
Dk 54, Ndemla anashindwa kufunga yeye akiwa na kipa tu, lakini akashindwa kufunga.

Dk 52 Miraji anafanya kazi ya ziada kuutoa mpira nje na kuwa kona, shambulizi halina madhara.
Dk 46, Simba wafanya sahambulizi na shuti alilopiga Okwi linaokolewa na kuwa kona isiyo na msaada.


MAPUMZIKO:

KIPINDI CHA KWANZA KIMEMALIZIKA KWA SARE YA BAO 1-1 HUKU SIMBA IKITANGULIA KUFUNGA BAO KUPITIA SHABANI KISIGA NA BAADAYE STAND KUSAWAZISHA MWISHONI.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic