January 21, 2015


Uongozi wa Klabu ya Yanga umefunguka kuwa unasubiria kuona Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), litachukua hatua gani kutokana na kitendo cha mshambuliaji wake Amissi Tambwe kukabwa koo na mchezaji wa Ruvu Shooting.


Tambwe alichezewa rafu kadhaa na beki wa timu hiyo, George Michael, mpaka akachanika mdomoni lakini mwamuzi hakuchukua hatua yoyote.

Katika mchezo wa Jumamosi kati ya Yanga na Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Taifa, kulikuwa na vurugu kiasi cha kufikia hatua mechi kusimama mara kwa mara.

Katibu  Mkuu wa Yanga, Dk Jonas Tiboroha, amefunguka kuwa wamesikitishwa na kitendo kilichotokea katika mchezo huo na kudai kuwa kuna matukio mengi ambayo hayakuwa sawa, hivyo wanawasubiri TFF kuona watachukua hatua gani kuhusiana na suala hilo.

“Hatukutaka kulizungumzia suala hili kwa watu na tulihitaji Watanzania waone wenyewe kama picha ilivyojieleza kwenye magazeti (anamaanisha Championi).

“Tunasubiri watu wenye dhamana ya mpira tuone watatoa maamuzi gani kuhusiana na mechi hiyo, kwani matukio mengi ambayo siyo mazuri yalijitokeza katika mchezo ule.

“Nadhani waamuzi wataandika ripoti yao, kamisaa wa mchezo pia ataandika na kila mmoja ameona, hivyo tunasubiri maamuzi yatakuwaje kwani kitendo kilichofanywa siyo kizuri na iwapo hakuna hatua watakayochukua tutajua cha kufanya,” alisema Tiboroha.

Alimalizia kwa kusema lengo ni kuhakikisha wachezaji wao wanakuwa na usalama kwa kutopatwa na matatizo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic