January 21, 2015

MBEYA CITY

Klabu ya Mbeya City, imetamba kuhakikisha inaendelea kupata ushindi katika mchezo wao ujao dhidi ya Tanzania Prisons.


Mbeya na Prisons zitavaana Jumamosi wiki hii katika mechi ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa kutokana na upinzani wa timu zote mbili.
 
PRISONS
Mbeya City kwa sasa ina alama 11 baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar wikiendi iliyopita na kwa sasa ipo katika nafasi ya 11, ingawa mwendo wa timu hiyo umeonekana kusuasua tofauti na msimu uliopita.

Ofisa habari wa  timu hiyo, Dismas Ten, alisema maandalizi yao yanakwenda vyema na lengo lao ni kuhakikisha wanaondoka na ushindi licha ya ligi kuonekana kuwa ngumu.

 “Tumejipanga vyema, ni mechi ngumu lakini tutapambana ili kuweza kuibuka na ushindi ili kuwa katika nafasi nzuri zaidi japo ni mchezo mgumu na wote tunakuwa katika uwanja wa nyumbani.

“Na kama mnanyofahamu Prisons kwa sasa siyo wa kubeza, ni timu nzuri sana, hivyo tunatakiwa kuwa makini sana,” alisema Ten.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic