February 24, 2015



Glavu alizovaa Muhammad Ali na Sonny Liston wakati wakipambana mwaka 1965 zimeuzwa kwa kiasi cha pauni 622,000 (zaidi ya Sh bilioni 1.5).


Glavu hizo alizivaa Ali wakati akimshinda Liston katika pambano kali lililobaki kuwa gumzo.

Pambano hilo lilifanyika Mei 25 kwenye Ukumbi wa American City of Lewiston, Maine nchini Marekani.

Licha ya mabondia hao kuwa na upinzani mkali na pambano hilo kuzungumzwa kwa kipindi kirefu, Ali alishinda kwa KO katika raundi ya kwanza.

Ngumi iliyomaliza pambano hilo katika raundi ya kwanza ilipewa jina la 'phantom punch' na hadi sasa ndiyo ngumi maarufu zaidi katika mchezo wa ngumi duniani.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic