Rais wa
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), amepeleka salamu za rambirambi kwa
familia ya Alex Massawe, kufuatia kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya
Taifa ya Tanzania (Taifa Star) na klabu ya Simba SC, Christopher Alex
kilichotokea jana mjini Dodoma.
Christopher
Alex Massawe aliwahi kuichezea timu ya Taifa, Taifa Stars mwanzoni
mwa miaka ya 2000 na kwa mafanikiko makubwa huku pia akiwa tegemeo katika
klabu yake ya Simba SC.
Katika salam
zake kwa familia ya Massawe, kwa niaba ya TFF, familia ya mpira wa miguu na Watanzania Rais Malinzi amewapa pole wapenzi wa mpira wa miguu nchini
katika kipindi hiki kigumu cha maombelezo.
0 COMMENTS:
Post a Comment