March 14, 2015

BANDA (KUSHOTO) AKIWA NA OWINO...
Kocha Mkuu wa Simba, Mserbia, Goran Kopunovic, ametamka kuwa mfumo wa kuanzisha viungo watatu katika timu hiyo utaendelea kutumika kutokana na kuwa na msaada mkubwa kwenye kikosi chake.


Tangu kuwasili kwa kocha huyo katika kikosi hicho, ameweza kukibadilisha katika mfumo wa kiuchezaji kutoka ule wa 4-4-2 uliokuwa unatumiwa na Mzambia, Patrick Phiri mpaka 4-3-3 ambapo viungo Abdi Banda na Jonas Mkude wamekuwa wakicheza kama wakabaji huku Said Ndemla akicheza kama mchezeshaji.

Kopunovic alisema ataendelea kutumia mfumo huo wa kuanzisha viungo watatu katika mechi zao kutokana na kuwa na faida.

“Nitaendelea kutumia mfumo wa 4-3-3 katika michezo yetu kutokana na kuwa na faida kubwa kwa upande wetu kwa sababu tunakuwa na uwezo wa kuwazuia wapinzani wetu kuanzia katikati ya uwanja.


“Vilevile mfumo huo umeonekana kueleweka na wachezaji wameuzoea kwa haraka zaidi, hivyo hakuna sababu yoyote ya kuachana nao kwani hata hivyo umetufikisha katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi kuu,” alisema Kopunovic.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic