Timu ya taifa ya wanawake (Twiga Stars), Ijumaa ijayo itashuka dimbani kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
kuwakarisbisha timu ya taifa ya wanawake ya Zambia 'The She-Polopolo'.
Twiga Stars
inayonolewa na kocha mkuu Rogasian Kaijage iliingia kambini mwishoni mwa wiki
na kikosi cha wachezaji 25 katika hostel za TFF zilizopo Karume, kujiandaa na
mchezo huo ambao ni muhimu wa kuwania kufuzu kwa fainali za michezo ya Afrika
mwaka huu.
Katika
mchezo wa awali uliofanyika wiki mbili zilizopita jijini Lusaka Zambia, Twiga
Stars iliibuka na ushindi wa mabao 4-2, mabao yaliyofungwa na Asha Rashid (2),
Shelder Boniface (1) na Sophia Mwasikili (1).
Mshindi wa
jumla katika mchezo huo atafuzu moja kwa moja kwa fainali za Michezo ya Afrika
zitakazofanya nchini Congo - Brazzavile kuanzia Septemba 13 mwaka huu.
0 COMMENTS:
Post a Comment