May 29, 2015


Kiungo wa Simba, Jonas Mkude, amesema amefurahishwa na kitendo cha kuitwa katika kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars, lakini akasisitiza kuwa bado hajui sababu za yeye kutoitwa awali.


Kocha wa Stars, Mart Nooij, hakumuita Mkude kikosini licha ya kuwa kwenye kiwango kizuri huku akigoma kutoa sababu na kudai kuwa Mkude ni mchezaji mzuri kwa makocha wengine siyo yeye, lakini amemuita kikosini katika kile kilichoonekana ni baada ya kupata presha kubwa kutoka kwa wadau mbalimbali waliohoji.

“Kuitumikia timu ya taifa ni jambo zuri na nimefurahi kwa kuwa uwezo ninao,” alisema Mkude.

Alipoulizwa kama ameambiwa sababu za kutoitwa awali, alisema: “Bado sijajua sababu, naamini kocha ndiye anafaa kujibu hilo swali, labda kuna kitu anaona kinapungua kwenye kikosi chake ndiyo maana ameamua kuongezea nguvu nyingine.”



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic