May 29, 2015

KISIGA (KUSHOTO) WAKATI AKIWA MTIBWA, HAPA AKIPAMBANA NA ATHUMANI IDD 'CHUJI'.

Klabu ya Mtibwa Sugar imeweka wazi msimamo wake kuwa ipo tayari kuwapokea wachezaji wake wote wa zamani ambao wanahitaji kurejea klabuni hapo, isipokuwa Shabani Kisiga kutokana na kuwa na rekodi mbaya ya nidhamu.


Kuna taarifa kuwa huenda wachezaji hao wakiwemo Hussein Javu, Nizar Khalfan wa (Yanga), Hussein Sharif ‘Cassilas’, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ (Simba) wanaweza kurejea klabuni hapo.

Ofisa Habari wa Mtibwa, Thobias Kifaru, amesema hivi:

“Wachezaji wanapoondoka Mtibwa si tatizo, jambo la msingi ni kufuata taratibu, ndiyo maana hatuwazuii kurejea lakini kwa Kisiga siyo rahisi kupokelewa kutokana na kuwa na makosa ya mara kwa mara.”

Aidha, Kocha Mecky Maxime ameshakabidhi ripoti yake klabuni hapo ambapo bodi itakutana Juni, mwaka huu kuijadili.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic