August 5, 2015

Mara tu baadaa ya Angel Di Maria kufuzu vipimo vya afya, neno la kwanza alilolisema ni kwamba anataka kuisaidia PSG katika michuano ya Ligi ya Mabingwa.


Di Maria amesema amekuwa na furaha kubwa kwamba anajiunga na timu hiyo ya Paris Saint-Germain lakini anachotaka ni kuona anakwenda mbali nayo katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Akisashaini, atakuwa mchezaji wa pili ghali zaidi nchini Ufaransa baada ya Edinson Cavani.

Cavani alisajiliwa kwa kitita cha euro milioni 64 wakati Di Maria itakuwa euro milioni 63.


Di Maria ameondoka Manchester United na kuzua gumzo kubwa kwa kuwa ilionekana kama hakutakiwa kuondoka wakati huu kwa kuwa timu hiyo ndiyo inajiweka vizuri ili kurejea katika hadhi yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic