August 5, 2015

Real Madrid imekubali kumuachia mshambuliaji wake Mfaranda, Karim Benzema, ajiunge na Arsenal.


Lakini imeweka wazi masharti kwamba kama kweli Arsenal iko tayari, basi ivunje rekodi yake ya usajili kwa kutoa pauni milioni 45.

Arsenal ndiyo iliweka rekodi ya manunuzi kwa Real Madrid baada ya kumchukua Mesut Ozil kwa kitita cha pauni milioni 42.5, hiyo ilikuwa mwaka 2013.
Sasa Madrid imesema hata Benzema, anaweza kuhamia London, England. Lakinia hayo ndiyo masharti.

Hivyo wakali hao wa Hispania, tayari wamerushia mpira upande wa Arsenal waliokuwa wakionekana kumtaka Benzema kwa muda sasa.


Kazi kwao kuucheza mpira huo kama kweli wanataka kumsajili Benzema ambaye hakika bado ni kifaa na Madrid wenyewe bado wanamtegemea.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic