Mshambuliaji mwenye
vituko wa Liverpool, Mario Balotelli amesherekea siku yake ya kuzaliwa kwa
kuwaalika wachezaji wenzake.
Balotelli
aliamua kutengeneza keki yenye jezi namba 9 ambayo huivaa anapokuwa timu ya
taifa ya Italia na si ile anayovaa Liverpool.
Ni mwaka wa 25
sasa kwake, na wachezaji walijitokeza katika mgahawa wa Sorrento kuungana naye,
baadhi wakiwa na familia zao.
Kati ya
walioungana na Balotelli ni pamoja na Lucas Leiva, Mamadou Sakho, Lazar
Markovic, Roberto Firmino, Divock Origi, Emre Can, Dejan Lovren na Martin
Skrtel.
0 COMMENTS:
Post a Comment