Rais wa TFF,
Jamal Malinzi ameendelea kusisitiza kwamba ikifikia siku akamnasa mtu
anayejihusisha na utoaji na upokeaji rushwa, atakuwa mfano kwa wengine wengi,.
Malinzi
ameiambia SALEHJEMBE kwamba ataendelea kulifuatilia suala hilo kwa karibu hadi
siku atakapomkamata mtu mmoja atakayekuwa mfano kwa wengine wasiotaka kuachana
na tabia hiyo.
“Rushwa ni
jambo baya, linatukwamisha na kuvuruga kabisa juhudi zetu za kukuza mpira. Wako
watu wanajihusisha na kila mara nimekuwa ninaonya.
“Inawezekana
ninavyoonya wako wanadhani ni utani. Lakini siku nitamkamata awe mwamuzi,
mchezaji au kiongozi, kwa kweli atajuta.
“Msisitizo
wangu ni watu kuachana na kujihusisha na masuala ya rushwa ili tuendeleze
mpira,” alisema Malinzi.
0 COMMENTS:
Post a Comment