Pamoja na kuichapa Prisons kwa mabao 2-0 jana,
Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema kuna mambo kadhaa ya
kurekebisha.
Pluijm amesema anataka kurekebisha mambo mengi
ambayo ameyaona katika mechi mbili za kirafiki kwa kuwa viwanja vya mikoani pia
hutoa taswira nzuri.
“Viwanja vingi vya mikoani si vizuri, mnapocheza
mechi utaona tofauti kubwa na mnapocheza Dar es Salaam.
“Hivyo bado kuna mambo kadhaa ya kurekebisha,
tutaendelea kufanya na kwa kuwa tutacheza na Mbeya City kwenye uwanja huo,
tutakuwa na nafasi ya kuyafanyia kazi tena ambayo tumerekebisha,” alisema
Pluijm.
Yanga tayari imecheza mechi mbili, ikianza na
Kimondo mjini Mbozi na kuifunga mabao 4-1 kabla ya kuichachafya Prisons kwa
mabao 2-0.
0 COMMENTS:
Post a Comment