Unaweza kusema ni uhakika tuzo ya mchezaji bora wa dunia Ballond’Or
inabaki Hispania.
Ligi yao ya La Liga inazidi kuonyesha ni bora zaidi kwa kuwa mmoja kati
ya Lionel Messi, Cristiano Ronaldo au Luis Suarez atakuwa mshindi.
Mshindi atatangazwa Agosti 27, wakati wa upangaji wa makundi wa michuano
mbalimbali ya Uefa.
Hapo wanachama 54 wa Uefa wanakutana kumaliza kazi hiyo.
Messi ambaye amebeba taji hilo mara nne anapewa nafasi zaidi. Mara ya
mwisho alilichukua 2011.
Baada ya hapo likahamia kwa Andres Iniesta (2012), Franck Ribéry (2013) na Cristiano (2014) ambaye
ndiye mtetezi.
0 COMMENTS:
Post a Comment