Malimi Busungu, amesema ana uhakika atasababisha mchezaji wa Azam FC kulambwa kadi nyekundu katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, leo.
Yanga na Azam zinakutana kwenye mchezo wa Ligi
Kuu Bara katika uwanja huo jijini Dar es Salaam, lakini Busungu amesema kwa
historia amekuwa akisababisha kadi nyekundu kila anapocheza dhidi ya Azam.
Busungu akiwa Mgambo JKT kabla ya kujiunga na
Yanga, msimu wa 20013/14 alisababisha kadi nyekundu kwa Erasto Nyoni
aliyemchezea vibaya, pia msimu uliopita Aggrey Morris alipatwa na tukio kama
hilo.
Mshambuliaji huyo amesema:
“Nina historia kila nikikutana na Azam katika ligi, mchezaji wao anapata kadi
nyekundu kwa kunichezea vibaya, natabiri Jumamosi (leo) itatokea hali hiyo.”
Busungu alisema anajua namna mabeki wa Azam
wanavyocheza kwa kutumia nguvu kupita kiasi lakini atahakikisha anafanya vizuri
mbele yao endapo atapata nafasi ya kucheza.
Wakati huohuo, Busungu alisema; “Nafurahi
kucheza pamoja na Ngoma kwani hata yeye ameniambia anapenda kucheza kikosi
kimoja na mimi kwa kuwa anavutiwa na uchezaji wangu wa kupambana.”
0 COMMENTS:
Post a Comment