MINGANGE AKIBADILISHANA MAWAZO NA MSHAMBULIAJI WAKE MPYA, HARUNA MOSHI 'BOBAN'. |
Kaimu Kocha Mkuu wa Mbeya Citym Meja Mstaafu
Abdul Mingange amefanya kitu kimoja cha kuwashtua wapinzani wake Simba katika
mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, leo.
Mingange ambaye anaiongoza Mbeya City kwa mara
ya kwanza akikaimu nafasi ya kocha mkuu baada ya kuondoka kwa Juma Mwambusi,
alisema amebadili mfumo wa ulinzi ili Simba isipate bao kirahisi.
Alisema: “Nitachezesha mabeki wa kati watatu
badala ya wawili kama ilivyozoeleka, unajua nataka tusifungwe kabisa na Simba
na hata tukiruhusu mabao basi yasiwe mengi ila lengo ni ushindi.”
Ili kutekeleza mpango huo, Mingange amepanga
kuwatumia mabeki Yohana Morris ambaye ni mdogo wa nyota wa zamani wa Prisons,
Osward Morris na Herry Morris na Haruna Shamte ambao watakuwa pamoja na kiungo
mkongwe Steven Mazanda.
“Mazanda ni kiungo lakini nitamtumia kama beki
wa kati anayechezesha timu huku akilinda sana, pale mbele watasimama Themi
Felix na Boban (Haruna Moshi) hapo kazi imeisha,” alisema Mingange aliyewahi
kuzinoa Ndanda FC na Villa Squad.
0 COMMENTS:
Post a Comment