Mshambuliaji Hamis Kiiza leo anaweza
akaitumikia timu yake kwenye Uwanja wa Sokoine wakati ikiivaa Mbeya City katika
mechi ya Ligi Kuu Bara.
Ingawa kumekuwa na taarifa kwamba Kiiza ni
majeruhi, taarifa za ndani kutoka Simba zimeeleza Kiiza tayari amerejea ingawa
wamekuwa hawataki kuweka mambo hadharani.
Imeelezwa Kiiza atakuwa kati ya wachezaji 11
watakaoanza leo katika kikosi cha Simba.
“Kama itashindikana, basi ataanzia benchi
lakini ana uhakika wa kuingia,” kilieleza chanzo.
“Juhudi kubwa za kimatibabu zimefanyika na sasa
Kiiza yuko katika hali nzuri.”
Kiiza raia wa Uganda ndiye mfungaji mwenye
mabao mengi zaidi Simba baada ya kuwa amepachika matano na ndiye anaongoza pia
katika waliofunga mengi katika Ligi Kuu Bara.
0 COMMENTS:
Post a Comment