Kamati
ya Taifa Stars chini ya Mwenyekiti, Faroukh Baghoza imekutana usiku huu katika Hoteli ya Serena jijini
Dar es Salaam.
Kamati
hiyo imekutana ikiwa ni kwa ajili ya kupanga mikakati pamoja na kuunda kamati
ndogondogo.
Kamati
hiyo pia ilitoa nafasi kwa wadau mbalimbali kwa ajili ya kutoa maoni yao kwa
lengo la kuhamasisha na kuisaidia Taifa Stars kuitoa Algeria katika mchakato wa
kuwania kucheza Kombe la Dunia, Novemba.
Stars
inawania kucheza Kombela Dunia nchini Urusi mwaka 2018 na sasa itakutana na
Algeria ikiwa ni baada ya kuitoa Malawi.
Katika
mkutano huo chini ya Baghoza na katibu, Teddy Mapunda, kamati hiyo iliwapa
wadau wakiwemo waandishi wa habari kutoa maoni yao katika masuala kadhaa
yakiwemo ya uhamasishaji kwa Watanzania.
Mengi
yalizungumziwa na baada ya hapo, mapendekezo hayo yatapelekwa kwenye kamati
ndogondogo ambazo zitagawanya majumu ili kuharakisha utendaji.
Lengo
kuu la kamati hiyo ni kusaidia kufanikisha ushindi kwa kuviong’oa vigogo,
Algeria ambao ndiyo timu bora Afrika kwa kipindi hiki.
SALEH ALLY 'JEMBE' NA EDO KUMWEMBE. |
KATABALO... |
IMANI MADEGA, MAULID KITENGE NA SALIM TRYAGAIN |
MSAFIRI MGOYI, BARAKA KIZUGUTO NA ISSAC CHANJI |
MOHAMMED NASSOR 'KIGOMA', PINTO NA WAMNBURA |
MULAMU NG'AMBI NA HASSAN |
0 COMMENTS:
Post a Comment