FRIENDS RANGERS... |
Ligi Daraja la Kwanza Tanzania (FDL) inatarajiwa kuendelea wikiendi
hii kwa michezo 12 kuchezwa katika viwanja mbalimbali kutoka katika makundi
yote matatu ya A, B, na C.
Ijumaaa African Lyon watakuwa wenyeji wa Polisi Dodoma katika
uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, ukiwa ni mchezo wa kundi A.
Jumamosi
Kundi A, Mjii Mkuu (CDA) watakua wenyeji wa Kiluvya Uinted katika uwanja wa
Jamhuri mjini Dodoma, KMC wakiwakaribisha Polisi Dar kwenye uwanja wa Karume
jijini Dar es salaam.
Kundi
B, Kimondo FC watawakaribisha Polisi Morogoro uwanja wa Vwawa – Mbozi,
Burkinafaso dhidi ya Kurugenzi uwanja wa Jamhuri Morogoro, Njombe Mji dhidi ya
JKT Mlale uwanja Amani Njombe.
Kundi
C, Mbao FC dhidi ya Panone FC uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, Rhino
Rangers dhidi ya Polisi Mara uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora, Geita Gold Vs
Polisi Tabora uwanja wa Nyankumbu Geita na JKT Kanembwa Vs JKT Oljoro uwanja wa
Jamhuri mjini Dodoma.
Ligi
hiyo itaendelea siku ya Jumapili kwa michezo miwili kuchezwa, Ashanti United
watawakaribsiha Friends Rangers uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, huku
Ruvu Shooting wakiwa wenyeji wa Lipuli FC katika uwanja wa Mabatini Mlandizi
mkoani Pwani.
0 COMMENTS:
Post a Comment