October 26, 2015


Kocha Mkuu wa Chelsea, Jose Mourinho sasa si siri tena kwamba amekalia kuti kavu.


Makocha Carol Ancelotti na Guud Hiddink ndiyo wanaopewa nafasi ya kuchukua nafasi yake.

Taarifa za ndani Chelsea zinaeleza kwamba uongozi w aklabu hiyo tayari umewasiliana na makocha hao na kuwaeleza kwamba wakae mkao wa kula.

Hali inaonekana si nzuri kwa Mourinho baada ya kupoteza mchezo dhidi ya West Ham kwa kuchapwa mabao 2-1 huku Mourinho akiondolewa benchi na mwamuzi na kulazimika kumalizia mechi hiyo akiwa jukwaani.



Taarifa nyingine zimeeleza Mourinho amepewa wiki moja tu na anaianza kesho katika mechi ya Capita One Stoke City.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic