FRIENDS RANGERS |
Ligi Daraja la Kwanza iliyoanza kutimua
vumbi Septemba 19, mwaka huu, imeonekana kuwa na washambuliaji wenye njaa ya
kufunga mabao kutokana na kwamba mpaka sasa mabao 109 yametiwa kimiani.
Mabao hayo yamefungwa huku ligi hiyo
ikiwa imeshamaliza raundi ya tano kwa timu zote 24 kushuka dimbani huku
ushindani ukionekana kuwa ni wa hali ya juu.
Cha kuvutia zaidi, timu zote nane
zilizogawanywa katika makundi matatu, makundi yao kama yanalingana kwani kwenye
mabao hayo 109, hayajapishana sana.
Kundi A, linaloongozwa na Ashanti United
yenye pointi 10, timu zake nane mpaka sasa zimeshafunga jumla ya mabao 37, huku
Kundi B linaloongozwa na Ruvu Shooting yenye pointi 10, lina jumla ya mabao 36,
sawa na Kundi C linaloongozwa na Geita Gold Sports yenye pointi tisa.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena
Oktoba 31, mwaka huu kwa kupigwa mechi 11 huku moja ikitarajiwa kupigwa siku
inayofuata kuhitimisha mzunguko wa sita.
0 COMMENTS:
Post a Comment