June 25, 2016


Wakati wowote kuanzia sasa Simba itamleta nchini straika Laudit Mavugo baada ya kumaliza mkataba wake kuitumikia Vital’O ya Burundi baada ya awali dili hilo kushindikana.

Tangu mwaka jana, Simba ilikuwa ikimuwania Mavugo raia wa Burundi kila kipindi cha usajili kinapofika lakini mambo huaribika na ikabidi isubiri hadi straika huyo alipomaliza mkataba wake.

Mmoja wa mabosi wa Kamati ya Usajili ya Simba ambaye hakutaka kutajwa jina, amesema Mavugo atatua wakati wowote kuanzia sasa na tayari alisaini mkataba wa miaka miwili tangu msimu uliopita.

Alisema mkataba huo uliigharimu Simba Sh milioni 36, lakini awali walibanwa na mambo ya mkataba wa straika huyo na timu yake hivyo kungoja hadi amalize mkataba.

“Mavugo atawasili nchini wakati wowote kuanzia sasa kwa kuwa ni mchezaji wetu na alisaini mkataba wa miaka miwili ya kuitumikia Simba na fedha zilizotumika kwenye usajili wake ni Sh milioni 36.

“Kwa sasa mkataba wake umekwisha kule katika timu yake aliyokuwa akiichezea, hivyo yupo huru na ni uhakika atatua kuja kuichezea Simba msimu ujao,” alisema bosi huyo. 

Mavugo ana uwezo mkubwa wa kuzifumania nyavu na Simba inaamini atakuwa mkombozi wao msimu ujao na kuzima ngebe za wapinzani wao.

SOURCE: CHAMPIONI




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic