February 28, 2017



Hali inaonekana kuwa si shwari kihivyo ndani ya klabu ya Yanga, hasa baada ya mashabiki wa klabu hiyo kumshambulia beki Vincent Bossou mtandaoni.


Mashabiki wa Yanga wanaonyesha kuchukizwa na Bossou kutokana na uamuzi wake wa kutotaka kucheza katika kikosi hicho.



Taarifa zinaeleza Bossou amegoma kucheza kwa kuwa anadai mshahara wake wa miezi kadhaa.


Lakini kupitia mtandao wa Instagram, Bossou amesema anaidai Yanga mshahara wa miezi minne.


Ingawa Bossou Kingereza chake ni cha "kuunga" amewajibu mashabiki wa Yanga, kwamba yuko tayari kuondoka ila wamlipe mshahara wake wa miezi minne.


Beki huyo raia wa Togo, tayari ametishia kuondoka Yanga, hali inayoonyesha mambo hayajakaa vizuri kwa kuwa mshambuliaji Donald Ngoma naye amekuwa akielezwa kuwa mgonjwa lakini kuna taarifa kuwa anafanya mgomo baridi.


1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic