June 25, 2017



Makamu wa Rais wa zamani wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Athumani Nyamlani amejitoa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania urais wa shirikisho hilo unaotarajiwa kufanyika Agosti 12, mwaka huu.


Nyamlani aliwasilisha barua TFF leo Jumapili Juni 25, mwaka huu ikiwa ni siku moja tu tangu Kamati ya Uchaguzi ipitishe jina lake kuwa miongoni mwa wagombea 10 wanaowania nafasi hiyo ya urais. Sababu aliyoeleza ni masuala binafsi.
 
Kwa msingi huo, wagombea wanaobaki kwenye kinyang’anyiro na kuhitajika kufika kwenye usaili kuanzia Juni 29, mwaka huu ni tisa wakiongozwa na Rais wa sasa, Jamal Malinzi anayetetea nafasi.
 
Mbali ya Malinzi wengine wanaowania nafasi hiyo ni Imani Madega, Wallace Karia, Fredrick Masolwa, Fredrick Mwakalebela, John Kijumbe, Shija Richard, Ally Mayay na Emmanuel Kimbe.
 
Waliojitokeza kuwania Makamu wa Rais na kurejesha fomu wako Mulamu Ng’hambi, Michael Wambura, Geofrey Nyange, Mtemi Ramadhani, Robert Selasela na Stephen Mwakibolwa.

Mbali ya nafasi za urais na makamu rais, Abdallah Mussa - aliyekuwa akiwania nafasi ya kugombea ujumbe wa Kamati ya Utendaji TFF kutoka Kanda Na. 1 (Mikoa ya Kagera na Geita) aliondolewa kwa sababu ya kutoambatanisha kivuli cha cheti ya elimu ya sekondari.

Hivyo wagombea wa nafasi za Wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa kufuata Kanda 13 ni kama ifuatavyo:

Kanda Na. 1 Mikoa ya Kagera na Geita;
     Soloum Chama
    Kaliro Samson
    Leopold Mukebezi

Kanda Na. 2 Mikoa ya Mara na Mwanza;
     Vedastus Lufano
    Ephraim Majinge
    Samwel Daniel
    Aaron Nyanda

 Kanda Na. 3 Mikoa ya Shinyanga na Simiyu;
     Benista Rugora
    Mbasha Matutu
    Stanslaus Nyongo
 
Kanda Na. 4 Mikoa ya Arusha na Manyara;
     Omari Walii
    Sarah Chao
    Peter Temu

 Kanda Na. 5 Mikoa ya Kigoma na Tabora;
     John Kadutu
    Issa Bukuku
    Abubakar Zebo
    Francis Michael
 
Kanda Na. 6 Mikoa ya Katavi na Rukwa;
     Kenneth Pesambili
    Baraka Mazengo

 Kanda Na. 7 Mikoa ya Mbeya, Songwe na Iringa;
     Elias Mwanjala
    Cyprian Kuyava
    Erick Ambakisye
    Abousuphyan Silliah

 Kanda Na. 8 Mikoa ya Njombe na Ruvuma;
     James Mhagama
    Golden Sanga
    Vicent Majili
    Yono Kevela
 
Kanda Na. 9 Lindi na Mtwara;
     Athuman Kambi
    Dunstan Mkundi
 
Kanda Na. 10 Mikoa ya Dodoma na Singida;
     Hussein Mwamba
    Mohamed Aden
    Musa Sima
    Stewart Masima
    Ally Suru
    George Benedict
 
Kanda Na. 11 Mikoa ya Pwani na Morogoro;
     Charles Mwakambaya
    Gabriel Makwawe
    Francis Ndulane
    Hassan Othman ‘Hassanol’

 Kanda ya 12. Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga
     Khalid Mohamed
    Goodluck Moshi
    Thabit Kandoro

 Kanda Na. 13 Mkoa wa Dar es Salaam
     Emmanuel Ashery
    Ayoub Nyenzi
    Saleh Alawi
    Shaffih Dauda
    Abdul Sauko
    Peter Mhinzi
    Ally Kamtande
    Said Tully
    Mussa Kisoky
    Lameck Nyambaya
    Ramadhani Nassib
    Aziz Khalfan
    Jamhuri Kihwelo
    Saad Kawemba
    Bakari Malima

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic