KARIA: KAIMU RAIS WA TFF |
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) inakutana leo saa 7 mchana.
Inakutana kujadili suala la uchaguzi baada ya kamati ya uchaguzi kuahirisha mchakato wa uchaguzi.
Kamati hiyo iliahirisha mchakato wa uchaguzi baada ya mwenyekiti wake kutofautiana na wajumbe waliokuwa wakitaka Jamal Malinzi lazima afanyiwe usaili licha ya kuwa mahabusu.
Kama haitoshi, Mwenyekiti wake, Waikili Revocatus Kuuli alisema wajumbe walitaka kuwakata baadhi ya wagombea bila sababu za msingi.
Hivyo akaona hakukuwa na suala la weledi na kuamua kusimamisha mchakato wa uchaguzi uliopangwa kufanyika Agosti 12 mjini Dodoma.
Hivyo, kamati ya utendaji ya TFF italisikiliza hilo na kufanya maamuzi ikiwa ni pamoja na kuamsha mchakato huo wa uchaguzi.
0 COMMENTS:
Post a Comment