Baada ya mjadala mrefu, uongozi wa Yanga umefanikiwa kumuongeza mkopo kiungo Mzimbabwe, Thabani Kamusoko.
Kamusoko ameongeza mkataba wa kuitumikia Yanga kwa miaka mingine miwili.
Mzimbabwe huyo kwa takribani wiki yote iliyopita alikuwa katika majadiliano na uongozi wa Yanga kuhusiana na mkataba wake mpya.
Leo kamati ya usajili imefanikiwa kumalizana naye na kasaini mkataba mpya mbele ya Katibu Mkuu, Charles Boniface Mkwasa.
0 COMMENTS:
Post a Comment