August 13, 2017




Pamoja kuvuliwa uanachama na kusimamishwa katika nafasi ya Mkuu wa Baraza la Wazee la Simba, Hamisi Kilomoni, ameonekana kushangazwa na taarifa hizo.

Mzee Kilomoni amesema hana taarifa zozote kuhuhusiana na suala hilo ambalo limefikiwa na wanachama wa Simba baada ya yeye kufungua kesi mahakamani akipinga mkutano.

Mkongwe huyo wa zamani wa Simba ambaye amekuwa akisigana na baadhi ya wanachama, amesema anayeondolewa kwenye udhamini anapaswa kuwa kuwa mgonjwa au mtu aliyehama zaidi ya mara moja jijini Dar es Salaam.

“Kweli sina taarifa lakini kuna taratibu za kufanya na si kama mnavyosema,” alisema.

Maana yake, mzee Kilomoni anaamini anaendelea kuwa mwenyekiti wa bodi ya wadhamini.

Wanachama baada ya kumsimamisha mzee Kilomoni uanachama, nafasi yake ameteuliwa kuishika Adam Mgoyi.


.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic