August 11, 2017



Kiungo mkabaji wa Yanga kutoka DRC Congo, Papy Kabamba Tshishimbi anatarajiwa kuwasili nchini leo Ijumaa kwa ajili ya kujiunga na timu hiyo.

Tshishimbi hivi karibuni alitua nchini na kusaini mkataba wa miaka miwili ya kuichezea timu hiyo kabla ya kurejea nyumbani kwao kwa ajili ya kumaliza matatizo ya kifamilia.

Awali, kiungo huyo alishindwa kujiunga na Yanga kutokana na mkataba wake kutomalizika katika kikosi cha Mbabane Swallows cha Swaziland.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Hussein Nyika amesema Tshishimbi alitakiwa ajiunge na timu tangu wiki hii ilipoanza lakini hati yake ya kusafiria (pasipoti) ndiyo ilikwamisha.


Aliongeza kuwa, mara baada ya kutua nchini, kiungo huyo atakuwepo kwenye kikosi kitakachoivaa Ruvu Shooting, kesho Jumamosi katika mechi ya kirafiki kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic