Stand United imeichapa Mbeya City kwa mabao 2-1 katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Kambarage.
Adam Salamba alianza kufunga bao mapema kipindi cha pili upande wa Stand United lakii Mohammed Samatta alisawazisha katika kipindi hicho.
Huku ikionekana kama mechi hiyo ingeisha kwa sare ya bao 1-1, Ally Ally aliifungia Stand United bao la pili katika dakika ya 62 na bao hilo lilidumu hadi mwisho wa dakika 90.
Kipindi cha kwanza mashambulizi yalikuwa ya zamu na ilikuwa vigumu nani angeshinda.
0 COMMENTS:
Post a Comment